Monday, July 30, 2018

Aslay Kumsaidia Enock Bella Kimuziki Kwa Kolabo.

Msanii wa Muziki wa Bongo fleva Aslay Isihaka amefunguka na kuweka wazi kuwa ana mpango wa kumshika mkono na kumsaidia Msanii mwenzake kutoka Yamoto Band Enock Bella.
Aslay alikuwa mmoja wa wasanii waliounda kundi la Yamoto Band lakini baada ya kundi hilo kuvunjika miaka michache iliyopita kila msanii alishika njia yake.
Baada ya kila msanii kuendelea na kazi zake binafsi Aslay alionekana kupata mafanikio makubwa zaidi lakini pamoja na Beka Flavor ambaye pia amekuwa anafanya vyema na Mbosso aliyesainiwa WCB amekuwa anafanya vizuri pia.
Lakini Enock Bella aliyekuwa maarufu kwa kuimba bezi kwenye Yamoto amekuwa akisuasua tofauti kabisa na wenzake kwani ameshatoa nyimbo kadhaa ambazo hazijafanya vizuri kabisa.
Kwenye mahojiano na kipindi cha Kikaangoni cha EATV, Aslay amefunguka na kukiri kuwa kuna jitihada anafanya kwa ajili ya kumsaidia msanii mwenzake Ikiwa ni pamoja na kolabo hivi karibuni:
Enock Bella alitangaza kusainiwa kwenye label iliyopo nchini Uganda mwaka jana mwishoni lakini baada ya muda mfupi akatangaza kujitoa.
in Entertainment
ASLAY NEWS
ENOCK BELLA NEWS
Ndio Enock Bella yupo na ninaongea naye na pia Bado Yupo Kwenye grupu moja kwaiyo bado tuna ukaribu na kuna jitihada tunafanya kwaiyo inshallah siku is nyingi mashabiki wataona kitu kutoka kwetu ingawa siwezi nikakiongelea sana”.

No comments:

Post a Comment

Una taarifa motomoto au sakata ambayo ungependa jeffawalamusic.blogspot.com nichapishe? Wasiliana nami kwa jeffawalamusic.blogspot.com, jeffawala@gmail.com , kwenye nambari: 0723410366 na kwenye facebook: jeff platnezz..

Do you have a hot story or scandal you would like me to publish, please reach me through jeffawala@gmail.com or telephone: 0723410366 and facebook: jeff platnezz jeffawalamusic.blogspot.com